Pages

Wednesday 1 July 2015

michuano ya kagame.yaiva ratiba kamili hii hapa,

 
 
 
 
 
 
 
 
 
KMKM vs TELECOM           
APR  vs  SHANDY               
YANGA vs GOR MAHIA       
Sun.19.7-2015
LLB AFC vs HEGAAN FC  
ADAMA CITY vs MALAIKA
AZAM  vs KCCA                 
Mon. 20.7.2015
TELECOM vs KHARTOUM-N  
GOR MAHIA vs KMKM 
Tue.21.7.2015
SHANDY vs LLB AFC      
HEGAAN vs  APR   
Malaika vs Azam        
Wed.22.7.2015
KHARTOUM vs KMKM
KCCA vs ADAMA City
TELECOM vs YANGA    
Thur.23.7.2015
HEGAAN vs SHANDY
APR vs LLB  AFC     
Fri.24.7.2015
KHARRTOUM-N vs GOR MAHIA
KMKM  vs YANGA
SAT.25.7.2015
KCCA vs MALAKIA
ADAMA CITY vs AZAM    
Sun.26.7.2015
GOR MAHIA vs TELECOM    
YANGA vs KHARTOUM-N    
Mon. 27. 7. 2015 Rest day
 Tue. 28.7.2015-Quarter-Final
B1 vs A3
A1 vs Best Qualifier
Wed. 29.7.2015
B2 vs C2
C1 vs A2
Thu. 29.7.2015 Rest Day
Fri. 31.7.2015- Semi finals
Winner 25 vs Winner 26
Winner 23 vs Winner 24
Sat.1.8.2015-Rest Day
Sun.2-8-2015- Final & 3rd Place Player
Loser 27 vs Loser 28
Winner 27 vs Winner 28

Friday 26 June 2015

Push Muziki Project 2015: Kwa Wale Wenye Vipaji vya Kuimba Sasa ni Zamu Yenu Kaa Mkao wa Kula

Kwa wale wasanii wachanga yaani Under Ground ni zamu yenu sasa Sbm Radio inakuletea bonge la Project ambayo yenye lengo la kuinua muziki wako….Sikiliza Sbm Radio Live kila siku za wiki kuanzia saa saba mchana na kuendelea 

kwa mawasiliano zaidi waweza piga simu namba +255 653 114 376 au +255 595 642 

Ukiona tangazo hili basi mwambie na mwenzako usiwe mchoyoooo hii ni Zamu yako nawe Kuwa Super Star

Friday 19 June 2015

Abramovich Avuruga Mipango ya Jose Mourinho

Mmiliki wa klabu ya Chelsea, Roman Abramovich amevuruga mipango ya kocha Jose Mourinho ya kutaka kipa wao mkongwe, Petr Cech ahamie nje ya England.

Badala yake, bilionea huyo wa Urusi ameamua kwamba Cech anayetaka kubaki London, akiwa na nia ya kukubali ofa ya Arsenal, aruhusiwe kutua Emirates.

Mourinho alikuwa anataka Cech asiuzwe kwa wapinzani wao wanaowania nao ubingwa msimu ujao, bali aende klabu nyingine kama Paris Saint-Germain (PSG) waliokwishaonesha nia ya kutaka kumsajili.

Watu wa ndani wa Chelsea wanasema kwamba Abramovich ameingilia kati mpango huo na kusema Cech aruhusiwe kwenda anakotaka, ikiwa ni kumpa heshima kwa kazi kubwa aliyowafanyia kwa miaka 11.

Tetesi za Soka Ulaya Leo Ijumaa 19.06.2015

Mshambuliaji kutoka Argentina anayechezea Manchester City Sergio Aguero amesema ametulia City licha ya Real Madrid kuonesha dalili za kumtaka.

Aguero, 27, anataka kuchukua Klabu Bingwa Ulaya na City (Daily Mirror) Paris St-Germain watapambana na Manchester City katika kumwania kiungo wa Juventus Paul Pogba, 22. 

PSG wapo tayari kutoa pauni milioni 70 wanazotaka Juve (Daily Star), winga wa Manchester United Nani, 28, aliyecheza kwa mkopo Sporting Lisbon msimu uliopita, atahamia Fenerbahce ya Uturuki kwa uhamisho wa pauni milioni 6 na mkataba wa miaka minne (Sun),


Thursday 18 June 2015

Kadi Nyekundu Yatibua Rekodi Brazili na Colombia

Ni zaidi ya miaka 24 timu ya taifa ya Colombia haijawahi kuifunga timu ya taifa ya Brazili katika mchezo wa soko.

Rekodi hiyo ilivunjwa jana usiku katika mchezo dhidi ya timu hizo mbili kivumbi cha michuano ya kombe Copa Amerika baada ya Wacolombia kuwafunga Wabrazuli kwa bao moja kwa nunge mnamo dadiki ya 36, bao lililowekwa kimiani na mchezaji Jeison Murillo.

Lakini tukio la kushangaza ni kadi mbili walizopata wachezaji Naymar (Brazil) na Carlos Bacca (Colombia) mnamo dakika za mwisho kabisa wakati refarii Enrique Osses Kutoka nchini Chile akipuliza firimbi kuashiria kwamba dakika za mchezo huo zimeisha.

Wakati refarii huyo akipuliza filimbi ya kumaliza mchezo huo, Mchezaj Naymar alipiga shuti kwa hasira na likatua mgongoni mwa mchezaji Carlos Bacca ambapo ilisababisha vurugu kubwa uwanjani hapo.

Aguero Akitua Madrid Inabidi Benzima Auzwe

Inasemekana kwamba kiwango anachokionyesha Sergio Aguero kwenye michuoano ya Copa Amerika kimewavutia mabosi wa Real Madrid na kushwawishika kutaka kusajili ndani ya klabu hiyo tajiri dunuiani.

Aguero kwa sasa anakipiga ndani ya klabu ya Manchester City ya Uingereza na mkataba wake unamuhitaji awepo ndani ya klabu hiyo mpaka mwaka 2019.

Madrid watalazimika kutoa kitika cha dola milioni 50 ili wampate kijana huyo ambaye msimu uliopita alikua mfungaji bora wa ligi ya Uingereza.

Kama hilo likitokea basi moja kwa moja mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema itabidi auzwe kwa maana mfumo wa kocha mpya wa Rafael Benitaz utamuweka Christian Ronald acheze namba tisa ambayo amnaicheza Benzama hivyo ni wazi kwamba Benzema atakaa benchi.

Klabu ya Real Madrid inamtaka mchezajiw a pembeni atakayeweza kucheza namba ya Christian Ronaldo, hivyo ikifanikiwa kuchukua Sergio Aguero ni wazi kwamba itabidi acheze winga ya Ronaldo.

Lakini hata hivyo huwenda hilo lisitokee kwani horodha ya majina kutoka kwa kocha Benitez haionyeshi kwamba jina la Aguero limo.

Kiungo wa Chile Arturo Vidal Ameachiliwa na Polisi Baada ya Kukamatwa

Kiungo wa Chile Arturo Vidal ameachiliwa na polisi baada ya kukamatwa kwa kosa la kusababisha ajali kwa madai wa ulevi. Vidal, 28, ambaye ndio anayeongoza kwa kufunga magoli katika michuano ya Copa America 2015 nchini mwake, Chile, alipata ajali na Ferrari yake usiku wa Jumanne. 

Leseni ya kuendesha gari ya Vidal aliyepata majeraha madogo, imesitishwa, lakini ataendelea kichezea Chile. "Nimewaangusha watu wote," alisema Vidal akibubujikwa na machozi baada ya kuachiliwa.